• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC TABORA AKAMILISHA AHADI MILIONI 15 KWA BONDIA ZUGO, PAMBANO KALI KATI YA ZUGO NA KUMAR KUFANYIKA KESHO TABORA HOTEL

Posted on: August 22nd, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Upendo Bert Wella, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Paulo Chacha, leo amemkabidhi bondia wa uzito wa kati, Abdul Zugo (Abdul Kessy Kasongo), fedha taslimu shilingi milioni 10. Fedha hizo ni sehemu ya ahadi ya shilingi milioni 15 aliyoitoa RC Chacha, ambapo tayari awali alimpatia shilingi milioni 5 kumwezesha maandalizi ya pambano kubwa la kuwania mkanda wa Ubingwa wa Mabara.

Zugo anatarajiwa kupanda ulingoni kesho, Agosti 23, 2025, dhidi ya bondia kutoka India, Sameer Kumar, katika pambano litakalofanyika majira ya jioni kwenye ukumbi wa Tabora Hotel, mjini Tabora.

Sambamba na tukio hilo la kukabidhi fedha, mabondia wote walipima afya na uzito kulingana na kanuni za Shirikisho la Ngumi Duniani (WBC), hatua muhimu kabla ya mashindano ya kimataifa.

Pambano hilo kubwa litapambwa na mapambano ya utangulizi yakihusisha mabondia kadhaa kutoka ndani na nje ya mkoa wa Tabora. Mojawapo ya mapambano yaliyovuta hisia ni kati ya Karim “Mtu Kazi” Mandonga na Juma Farahani, ambao leo walitambiana vikali wakati wa upimaji wa afya na uzito, hali iliyoongeza hamasa na mvuto wa mashindano hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Wella, amewataka wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushuhudia pambano hilo la kihistoria, huku akisisitiza umuhimu wa kuwaunga mkono vijana wa Kitanzania wanaopeperusha bendera ya taifa kupitia michezo ya ngumi.

“Huu ni wakati wa kuonyesha mshikamano wetu kama Watanzania. Vijana wetu kama Abdul Zugo na Juma Farahani wanapigania heshima ya mkoa wa Tabora na taifa kwa ujumla, hivyo tushiriki kuwatia moyo,” alisema.

Wakazi wa Tabora na vitongoji vyake wanatarajiwa kufurika ukumbini kushuhudia burudani hii kabambe, ambapo ushindi wa mabondia wa ndani unaweza kufungua milango mipya ya kimataifa kwa mchezo wa ngumi nchini Tanzania.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TABORA AKAMILISHA AHADI MILIONI 15 KWA BONDIA ZUGO, PAMBANO KALI KATI YA ZUGO NA KUMAR KUFANYIKA KESHO TABORA HOTEL

    August 22, 2025
  • “KANISA LIPO TAYARI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUENDELEZA MAENDELEO TABORA: KARDINALI RUGAMBWA”.

    August 11, 2025
  • TFS YAENDESHA MAFUNZO YA UHIFADHI WA MAZINGIRA DHIDI YA UHARIBIFU WA ARDHI NA MISITU MKOANI TABORA

    August 11, 2025
  • MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MAGHARIBI YAFIKIA TAMATI: BALOZI SIRRO AHAMASISHA WAKULIMA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YAO KWA KUTUMIA VIFUGASHIO BORA.

    August 08, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa