• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

DKT. BATILDA ATEMBELEA MAJERUHI WA AJALI YA NZEGA

Posted on: October 24th, 2023

Leo Oktoba 24, 2023, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian ametembelea Hospitali ya Wilaya ya Nzega na Hospitali ya Rufaa ya Nkinga na kuwajulia hali majeruhi, ndugu, jamaa na marafiki waliopoteza ndugu na jamaa zao kwenye ajali ya basi na lori iliyotokea Oktoba 21, 2023, kata ya Uchama, Wilayani Nzega.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa Hospitali ya Wilaya  ya Nzega akiongea na baadhi ya Ndugu na Jamaa wanaosubiri kusafirisha miili ya ndugu na jamaa zao waliopoteza maisha kwenye ajali ya basi na roli iliyotokea Oktoba 21, 2023.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwafikisha salamu za pole kutoka kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa baadhi ya wajeruhi waliopata ajali ya Basi na Lori Oktoba 21, 2023 Kata ya Uchama Wilayani Nzega.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akitoa mkono wa pole na kuwajulia hali  baadhi ya majeruhi wa ajali ya Basi na Lori kwa kuwapatia kiasi kidogo cha fedha na Asali kwa ajili ya kutibu majeraha waliyoyapata.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwasili Hospitali ya Rufaa ya Nkinga iliyopo Wilayani Igunga, kwa ajili ya kuwaona na kuwajulia hali Majeruhi wa ajali ya basi wanaoendelea na matibabu hospitalini hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiongea na vyombo vya habari alivyoambata navyo, ambapo sehemu kubwa amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuhimarisha miundombinu ya Afya, Wilayani Igunga na Nzega ambayo imesaidia kutoa huduma za dharura kwa baadhi ya majeruhi.

Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amewahakikishia majeruhi wote, kwamba Serikali imehakikisha majeruhi wanapatiwa matibabu kwa uharaka na umakini wa hali ya juu, na gharama zote zitalipwa na Serikali kwa kushirikiana na mmiliki wa mabasi wa kampuni ya Alfa.

Pia Mkuu wa Mkoa ametoa pongezi kwa madaktari, wauguzi na watendaji wa Serikali pamoja na Jeshi la Polisi waliojitoa na kuhakikisha wanaokoa maisha ya watanzania waliopata ajali. Bila kusahau wananchi na Vyombo vya habaroi vilivyotumia muda usiku na mchana kuhabarisha Umma kuhusiana na ajali hiyo mbaya iliopoteza maisha ya watanzania wenzetu.


Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa, mpaka sasa kati ya majeruhi 60 waliofikishwa hospitalini hapo, wamebaki 19 na wote wanaendelea vizuri na madaktari wanafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha wanapata unafuu. Kuna majeruhi wawili wapo Bugando nao pia wanaendelea vizuri. 


Aidha kwenye ajali hiyo watu 18 walipoteza maisha papo hapo, na miili 13 tayari imekwishatambuliwa na tayari imeshachukuliwa na wanandugu, na mpaka sasa bado miili 5 ambayo tunaendelea kuwatafuta ndugu na jamaa zao ili kuhakikisha waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo wanasitiriwa.


Ikumbukwe kuwa, majira ya saa 5 asubuhi Oktoba 21, 2023 Kata ya Uchama, Wilayani Nzega majira ya saa 5 asubuhi Oktoba 21, 2023 kulitokea ajali iliyohusisha Basi la Abiria, Kampuni ya Alfa lenye namba ya usajili T 612 CQD na Lori la mafuta, Kampuni ya GBP lenye namba ya usajili T.526 AEB  na kusababisha vifo 18 na majeruhi 60 ambao wote walifanikiwa kupata matibabu.


Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa