• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

JESHI LA POLISI TABORA LAPATA MAGARI 6 MAPYA KWA AJILI YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

Posted on: May 12th, 2025

Katika juhudi za kuimarisha utendaji kazi wa Jeshi la Polisi nchini, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mheshimiwa Paulo Matiko Chacha, amekabidhi rasmi magari sita aina ya Toyota Land Cruiser kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP) Richard Abwao.

Hafla hiyo imefanyika katika uwanja wa nje ya Ofisi ya Ukumbi wa Mikutano wa Chief Isike Mwanakiyungi, Tabora, ambapo magari hayo yametolewa kwa ajili ya kusaidia kazi za doria, misako na oparesheni mbalimbali za kiusalama katika mkoa huo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo, RC Chacha amesema:

“Magari haya ni kwa ajili ya kuimarisha utendaji wa Jeshi letu la Polisi. Mheshimiwa Rais ataendelea kuleta magari zaidi kwa ajili ya idara ya upelelezi na vikosi vya FFU katika wilaya zote. Ni wajibu wetu kuyatunza magari haya na kuhakikisha yanatumika kwa kazi maalum zilizokusudiwa. Tuendelee kuwalinda wananchi wa Tabora, ambao tumekabidhiwa jukumu la kuhakikisha usalama wao wakati wote.”

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, SACP Richard Abwao, ameishukuru serikali kwa msaada huo akisema:

“Kupokea magari haya sita kutoka kwa Mkuu wa Mkoa ni faraja kubwa kwetu. Magari haya yatagawanywa kwa wakuu wa polisi wa wilaya zote, jambo litakalopunguza kwa kiasi kikubwa changamoto tulizokuwa nazo. Namshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutupatia magari haya, pamoja na IGP kwa kutugawia, na Mheshimiwa Chacha kwa kuyakabidhi rasmi hapa Tabora. Tumejipanga kuhakikisha magari haya yanatunzwa na kutumika ipasavyo kwa malengo yaliyokusudiwa.”

Magari haya yanatarajiwa kuongeza ufanisi katika shughuli za kiusalama mkoani Tabora, ikiwa ni pamoja na kuwezesha doria za mara kwa mara, oparesheni za kiintelijensia na kuimarisha uwezo wa kuwahudumia wananchi kwa haraka zaidi.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WIZARA YA AFYA NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA TABORA YAENDESHA KIKAO ELEKEZI CHA MREJESHO WA MAFUNZO NA MAPITIO YA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

    May 14, 2025
  • JESHI LA POLISI TABORA LAPATA MAGARI 6 MAPYA KWA AJILI YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

    May 12, 2025
  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa