• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

Posted on: May 3rd, 2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko ameongoza hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa kiwanda kipya cha kuzalisha nguzo za zege cha TCPM (Tanzania Concrete Poles Manufacturing Company Limited), kilichopo mkoani Tabora – hatua kubwa katika safari ya Tanzania kuelekea kuwa na uhakika wa nishati ya umeme.

Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja Mkuu wa TCPM, Ndg. Yusuph Kitivo alieleza kuwa ujenzi wa kiwanda hicho ulianza rasmi tarehe 30 Oktoba 2024, mara baada ya kusainiwa kwa mkataba baina ya kampuni hiyo tanzu ya TANESCO na wakandarasi wazawa — Msangi Enterprises na Bahari Construction Company Ltd.

Mradi huo unaogharimu shilingi bilioni 6.8 umefikia asilimia 75 ya utekelezaji, na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Juni 2025. Kufuatia ukamilikaji wake, kiwanda hicho kitaanza uzalishaji rasmi mwezi Julai mwaka huu, kikitarajiwa kuzalisha wastani wa nguzo 120 kwa siku. Hii ni sehemu ya juhudi za serikali ya awamu ya sita kuhakikisha nchi inakuwa na mfumo madhubuti wa usambazaji wa nishati kwa kutumia vifaa vya kudumu na vya kisasa.

Akitoa salamu za chama, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Ndg. Said Nkumba, aliipongeza wizara ya Nishati kwa jitihada inazozifanya katika kusambaza umeme vijijini na mijini. Alisisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa mstari wa mbele kuwaletea wananchi maendeleo na kuwapatia wagombea wanaokubalika na jamii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha, alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea mkoani humo, akisema mradi huo utazalisha ajira na kuchochea uchumi wa wananchi wa Tabora.

Wabunge wa mkoa huo pia walitoa shukrani zao kwa serikali, huku Mhe. Munde Tambwe (Mbunge wa Viti Maalum) akiomba serikali kuanzisha kiwanda cha kuchakata tumbaku na kufufua kiwanda cha nyuzi, akibainisha kuwa Tabora ina uzalishaji mkubwa wa tumbaku na pamba. Naye Mhe. Emmanuel Mwakasaka (Mbunge wa Tabora Mjini) aliitaka serikali kutazama upya gharama za kuunganisha umeme kwa wakazi wa vijijini, hususan maeneo ya pembezoni mwa mji wa Tabora.

Akihutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria hafla hiyo, Mhe. Dkt. Biteko aliipongeza serikali ya awamu ya sita kwa jitihada kubwa za kuimarisha sekta ya nishati. Alisisitiza kuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anatamani kuona matokeo halisi, si maneno matupu, katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Ametoa rai kwa wananchi kuanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa ajili ya kulinda afya zao na kuhifadhi mazingira. Aidha, alikumbusha umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi kwa kujitokeza kujiandikisha, kuhudhuria kampeni kwa amani, na hatimaye kupiga kura kwa kuzingatia sera na kazi za wagombea badala ya matusi na mipasuko ya kisiasa.

Hafla hii imehitimisha ziara ya siku mbili ya Naibu Waziri Mkuu mkoani Tabora, ikiwa ni sehemu ya msisitizo wa serikali katika kuimarisha miundombinu ya nishati nchini kwa maendeleo endelevu.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WIZARA YA AFYA NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA TABORA YAENDESHA KIKAO ELEKEZI CHA MREJESHO WA MAFUNZO NA MAPITIO YA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

    May 14, 2025
  • JESHI LA POLISI TABORA LAPATA MAGARI 6 MAPYA KWA AJILI YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

    May 12, 2025
  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa