• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAZIRI SHEMDOE ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO YA SH. BILIONI 17.2 MKOANI TABORA, ATOA WITO IKAMILIKE KWA UBORA NA KWA WAKATI

Posted on: January 25th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, amempokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, mkoani Tabora kwa ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa mkoani humo.

Awali akitoa taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Tabora, Katibu Tawala wa Mkoa, Dkt. John Mboya, amesema mkoa umeendelea kupata mafanikio makubwa katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu, afya, miundombinu pamoja na eneo la ukusanyaji wa mapato. Kwa upande wa sekta ya elimu, Mkoa wa Tabora umefanikiwa kupata matokeo mazuri ya Kidato cha Sita kwa asilimia 99 na kushika nafasi ya pili kitaifa.

Katika sekta ya afya, Dkt. Mboya amesema Mkoa wa Tabora umefanikiwa kujenga hospitali za wilaya katika wilaya zote, pamoja na kuongeza vituo vya kutolea huduma za afya kutoka vituo 348 mwaka 2021/2022 hadi kufikia vituo 460 mwaka 2024/2025. Aidha, vituo vya kutoa huduma za upasuaji wa dharura kwa wajawazito vimeongezeka kutoka 25 mwaka 2021/2022 hadi kufikia 40 mwaka 2024/2025, sambamba na kuboreshwa kwa miundombinu ya kutolea huduma za afya ikiwemo Jengo la Wagonjwa Mahututi na Jengo la Wagonjwa wa Dharura.

Katika ziara hiyo, Mhe. Prof. Shemdoe alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa bwalo la chakula katika Shule ya Sekondari Tabora Wavulana unaogharimu shilingi milioni 200, mradi wa ujenzi wa barabara ya Mailitano yenye urefu wa kilomita 2.418 kwa kiwango cha lami, sehemu ya mradi wa TACTIC unaojumuisha jumla ya kilomita 10.7 kwa gharama ya shilingi bilioni 16.4, pamoja na mradi wa upanuzi wa Kituo cha Afya Mailitano unaogharimu shilingi milioni 675.

Baada ya kukagua miradi hiyo, Mhe. Prof. Shemdoe ameonesha kuridhishwa na utekelezaji wake na kutoa wito kwa wasimamizi kuhakikisha miradi inajengwa kwa viwango bora vinavyokidhi thamani ya fedha na kukamilishwa kwa wakati ili ianze kutoa huduma kwa wananchi. Aidha, amewaelekeza watendaji wa serikali kote nchini kuepuka matumizi yasiyo ya lazima na kuelekeza rasilimali zaidi kwenye miradi ya maendeleo ili kutimiza azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuwaletea wananchi maendeleo na ustawi.

Vilevile, Mhe. Prof. Shemdoe ameelekeza ujenzi wa miradi ya maendeleo uzingatie kikamilifu sheria na masharti ya mikataba, sambamba na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wakandarasi wazembe wanaochelewesha utekelezaji wa miradi, ikiwemo kuwakata sehemu ya fedha za malipo yao, kama ilivyofanyika kwa mkandarasi anayetekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya Mailitano.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAZIRI SHEMDOE ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO YA SH. BILIONI 17.2 MKOANI TABORA, ATOA WITO IKAMILIKE KWA UBORA NA KWA WAKATI

    January 25, 2026
  • MWL. RWEYEMAMU AFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYANI SIKONGE, AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA KUFANYA TATHMINI YA MATOKEO YA KITAIFA YA MWAKA 2025.

    January 23, 2026
  • WASHIRIKI KUTOKA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI - TANZANIA WAHITIMISHA ZIARA YAO MKOANI TABORA KWA KUTEMBELEA KIWANDA CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI SIKONGE

    January 17, 2026
  • WASHIRIKI WA KOZI YA 14 CHUO CHA ULINZI WA TAIFA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO KWA VITENDO MKOANI TABORA

    January 15, 2026
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa