Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian ameeleza kuwa, jumla ya madaktai bingwa kumi (10) wameshawasili Mkoani Tabora kwa ajili ya kutoa huduma ya magonjwa ya moyo kwa muda siku tano (5) kuanzia leo Januari 15, hadi Januari 19. Ambapo ametoa wito kwa wananchi wa Tabora kujitokeza na kupata huduma hiyo.
Katika kuhakikisha huduma za magonjwa ya moyo zinawafikia wananchi Mkoani Tabora Timu ya madaktari bingwa kumi (10) wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JKCI) wamewasili Mkoani Tabora kwa ajili ya kutoa huduma za magonjwa ya moyo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora Kitete kwa lengo la kutoa huduma kwa takribani siku tano (5).
Mganga mkuu wa Mkoa wa Tabora Dk. Honoratha Rutatinisibwa amesema ujio wa madaktari hao utawapunguzia wananchi wa mkoa huo gharama za kusafiri na kwenda Mikoa mingine ya mbali kutafuta matibabu ya kibingwa mbali na mkoa huo.
Hata hivyo Mganga mfawidhi wa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete DK. Mark Waziri amesema watalaamu hao watasaidia pia kutoa ujuzi kwa madaktari wengine waliopo katika hospitali ya Rufaa ya Kitete ambao pia watashirikiana moja kwa moja na daktari hao bingwa. Ametoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Afya kwa kufanikisha madaktari hao wanafika mkoani tabora na kutoa huduma hiyo.
Loveness Mfanga ambaye ni kiongozi wa jopo la madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo amezibainisha baadhi ya huduma zitakazotolewa na madaktari hao ikiwa ni pamoja na magonjwa ya kuta za moyo na utafiti wa magonjwa ya moyo na lishe.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa