• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MHE. CHACHA, AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA ELIMU KATA NA WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI MKOA WA TABORA.

Posted on: January 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Matiko Chacha, amefungua kikao kazi cha maafisa elimu kata na wakuu wa shule za sekondari mkoa wa Tabora kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Tabora, Isike Mwanakiyungi. Kikao hicho ni cha siku mbili, na lengo lake kuu ni kuwajengea uwezo walimu wakuu pamoja na maafisa elimu kata ili kuboresha taaluma mkoani Tabora.

Katika ufunguzi wa kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi  Elimu, Bi. Upendo Rweyemamu, ameipongeza na kuishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya elimu, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule za msingi na sekondari katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Tabora. Amesema kuwa juhudi hizi zimeleta mabadiliko chanya katika mazingira ya utoaji elimu, na kwamba wanafunzi sasa wanapata mazingira bora zaidi ya kujifunza.

Hata hivyo, Bi. Rweyemamu amekiri uwepo wa  changamoto zinazoukabili mkoa katika sekta ya elimu. Amebainisha kuwa utoro na mdondoko wa wanafunzi ni miongoni mwa sababu kubwa zinazozorotesha maendeleo ya elimu na ufaulu mkoani Tabora pamoja  ushirikiano hafifu kutoka kwa wazazi, hasa katika suala la kuchangia chakula shuleni, umeendelea kuwa kikwazo kikubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunza.

Katika hatua nyingine, Mhe. Paul Chacha ametoa pongezi kwa walimu kwa juhudi zao katika kudhibiti vitendo viovu, ikiwemo ukatishaji wa elimu kwa watoto wa kike, vitendo ambavyo vinavunja maadili ya jamii. Amesisitiza kwamba walimu wanajukumu la kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto wote wanapata elimu bila vikwazo vya kijinsia au kijamii.

Akizungumzia changamoto ya utoro na mdondoko, Mhe. Chacha ametoa agizo kwa kila mzazi mwenye mtoto wa umri wa kwenda shule ahakikishe anahudhuria shule mara tu zitakapofunguliwa. Amesema kuwa atakayeshindwa kutekeleza wajibu huo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Aidha, Mhe. Chacha amewasihi walimu kudumisha umoja na mshikamano katika kazi zao, akisisitiza kuwa umoja ndio nguzo ya mafanikio. Ametoa wito kwa walimu kutojiingiza katika migawanyiko ya ndani na kuwa na kauli moja katika kutatua changamoto zinazojitokeza. "Msifikiri ni sifa kutengana, jitahidini sana muwe na kauli moja, chagueni wawakilishi wenye kuwaunganisha na wala msikubali kushusha thamani yenu kwa vitu vidogo, Walimu hamuwezi kuwa na sauti moja yenye nguvu mkiwa mmemeguka vipande vipande.”amesisitiza.

 Kikao kazi hiki kinatarajiwa kutoa ufumbuzi wa haraka kwa changamoto mbalimbali zinazoukabili mkoa katika sekta ya elimu na kujenga uwezo kwa walimu na maafisa elimu kata katika kuhakikisha maendeleo ya elimu yanafikiwa kwa haraka.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa