• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MHE, CHACHA AKEMEA UZEMBE NA KUTOWAJIBIKA KWA BAADHI YA WATUMISHI WA SHULE YA WASICHANA TABORA

Posted on: June 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, ametembelea Shule ya Wasichana Tabora kwa lengo la kuzungumza na uongozi wa shule hiyo pamoja na wazazi, kufuatia mfululizo wa matukio yaliyoibua sintofahamu kuhusu mwenendo wa nidhamu na uongozi katika shule hiyo ya kihistoria.

.

Akitoa taarifa rasmi ya uchunguzi, Katibu Tawala wa Mkoa, Dkt. John Mboya, alieleza kuwa mwanafunzi wa shule hiyo ambaye jina lake na taarifa zake zimehifadhiwa kwa mujibu wa sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, mwanafunzi huyo alitoa taarifa ya kuumwa na akapelekwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa Kitete,lakini baada ya kupokelewa, kabla majibu ya vipimo vyake kutoka alibainika kuwa alijifungua katika maliwato ya hospitalini hapo hali ambayo iliulazimu uongozi wa wilaya na mkoa ukiongozwa na Katibu Tawala mkoa kuunda timu maalum kufanya uchunguzi juu ya hali hiyo na mwenendo mzima wa uendeshaji wa shule hiyo.


Taarifa ya uchunguzi ilibaini kuwa mwanafunzi huyo aliripoti shuleni hapo akiwa na ujauzito—lakini cha kushtua zaidi ni kuwa hakuna mwalimu wala kiongozi yeyote wa shule aliyeweza kugundua hali hiyo hadi kufikia hatua ya kujifungua.

 “Tabia ya baadhi ya wanafunzi kujihusisha na ngono wakiwa bado shuleni ni jambo linaloumiza sana. Wazazi tunapaswa kushirikiana kwa nguvu katika malezi ya watoto wetu wa kike.”Alieleza Dkt. Mboya

Uchunguzi huo pia ulibaini kuwa hali ya utendaji shuleni hapo imeathiriwa na hali ya baadhi ya walimu kukaa kwa muda mrefu katika kituo kimoja cha kazi bila uhamisho hali ambayo imesababisha mazoea, kuvuja kwa maadili ya kazi, na kudhoofisha uongozi.


Akizungumza mbele ya walimu na wazazi wa shule hiyo, Mhe. Paul Chacha hakuficha masikitiko yake kuhusu hali ya shule hiyo:


“Kama mtu ana miaka 17 hapa,hii ina maana ni umri wa tangu mtoto anazaliwa mpaka anafika kidato cha sita, alishazoea hata darasani haendi, hana haja ya kujua nidhamu ya mtoto ikoje, mwalimu wa darasa haingii na hana haja ya kujua darasa hilo linaendeleaje? Tatizo lililopo ni watu kufanya kazi kwa mazoea,” Mhe. Chacha alisema kwa masikitiko.


Mhe. Chacha alitoa maagizo ya kuwa walimu wote waliodumu shuleni hapo  kwa muda mrefu bila kuhamishwa wachukuliwe hatua za kupelekwa vituo vingine vya kazi. Mhudumu wa afya aliyehusika na ujazaji wa fomu ya uchunguzi wa afya ya mwanafunzi huyo achukuliwe hatua za kisheria kwa uzembe aliouonesha. Ufuatiliaji wa karibu ufanyike ili kubaini aliyesababisha ujauzito wa mwanafunzi huyo na sheria ichukue mkondo wake.


Vilevile Binti huyo arejee shuleni mara tu baada ya kumaliza mapumziko ya uzazi, ili aendelee na masomo yake kama inavyoelekezwa na sera ya elimu jumuishi.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Uyui ambaye pia anakaimu Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Mohamed Mtulyakwaku, alimshukuru Mhe. Chacha kwa kuchukua hatua stahiki na kuwaasa walimu kuzingatia wito wao na kufanya kazi njema waliyoitiwa na Mwenyezi Mungu ya kuelimisha dunia kwa upendo na bidii.


Ziara hii imeacha ujumbe mzito kwa viongozi wa shule, jamii na serikali kwa ujumla kuhusu umuhimu wa malezi ya watoto wa kike, ufuatiliaji wa karibu wa maendeleo yao, na uwajibikaji usioyumba kutoka kwa walimu na watumishi wa umma.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE, CHACHA AKEMEA UZEMBE NA KUTOWAJIBIKA KWA BAADHI YA WATUMISHI WA SHULE YA WASICHANA TABORA

    June 10, 2025
  • MSAADA WA TREKTA KUTOKA SERIKALINI KUFUNGUA MILANGO YA KITIVO CHA KILIMO NA MAZINGIRA AMUCTA – MHE. CHACHA AONGOZA HAFLA YA MAKABIDHIANO.

    June 10, 2025
  • WATUHUMIWA 11 MBARONI KWA KUJIHUSISHA NA KILIMO CHA BANGI KATIKA ENEO LA HIFADHI YA MTO IGOMBE – TABORA.

    June 09, 2025
  • TABORA YAHITIMISHA MASHINDANO YA UMISSETA: MANISPAA YA TABORA YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA KATIKA MASHINDANO HAYO NGAZI YA MKOA

    June 06, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa