• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WATUHUMIWA 11 MBARONI KWA KUJIHUSISHA NA KILIMO CHA BANGI KATIKA ENEO LA HIFADHI YA MTO IGOMBE – TABORA.

Posted on: June 9th, 2025

Katika hatua ya kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mheshimiwa Paulo Chacha, ameongoza oparesheni maalum ya kuteketeza mashamba ya bangi yaliyogundulika ndani ya hifadhi ya mto Igombe, iliyopo katika Manispaa ya Tabora.

Oparesheni hiyo, ambayo imesheheni ushirikiano kati ya viongozi wa serikali, jeshi la polisi,jeshi la akiba na mamlaka ya kudhibiti dawa za kulevya, imelenga kusafisha eneo hilo na kufikisha ujumbe mkali kwa wale wote wanaojihusisha na kilimo haramu cha bangi.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mhe. Chacha alielezea kwa ukali kutoridhishwa na tabia ya baadhi ya wananchi wanaovamia maeneo ya hifadhi na kuendesha shughuli haramu za kilimo cha bangi.

“Bangi ni zao haramu ambalo linaangamiza vijana wetu na kuharibu nguvu kazi ya taifa. Serikali na jamii kwa ujumla hatuwezi kulikubali hili. Natoa onyo kali kwa wote wanaojihusisha na kilimo hiki waache mara moja,” alisisitiza Mhe. Chacha, akiongeza kuwa kuishi hifadhini na kulima bangi ni makosa mawili makubwa ya kisheria.

Katika oparesheni hiyo, Jeshi la Polisi mkoani Tabora limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 11 – wanaume 9 na wanawake 2 – waliokutwa wakiendesha shughuli za kilimo cha bangi katika eneo hilo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Richard Abwao, alieleza kuwa tayari wamekamata magunia 25 ya bangi katika oparesheni hiyo.

 “Tutahakikisha wauzaji wakubwa wa bangi wanakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria. Huu ni mwanzo wa oparesheni endelevu,” alisema Kamanda Abwao. Alitoa rai kwa wananchi kuachana na kilimo haramu na kuhamasisha shughuli halali za kiuchumi.

Kwa upande wake, Afisa Oparesheni kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Nchini, Ndg. Godfrey Renatus, ameeleza kuwa zaidi ya ekari tano za mashamba ya bangi zimeteketezwa katika oparesheni hiyo. Alisisitiza kuwa sheria itachukua mkondo wake kwa wote wanaobainika kujihusisha na biashara hiyo haramu.

“Tunaomba wananchi washirikiane nasi kwa kutoa taarifa kupitia namba 119. Usiri wa taarifa zao utahakikishwa kikamilifu,” alisema Ndg. Renatus.

Mapambano dhidi ya dawa za kulevya yameendelea kuwa kipaumbele kwa serikali na mamlaka zake, huku wito ukiendelea kutolewa kwa jamii kushiriki kikamilifu kuokoa kizazi kijacho kutokana na madhara ya matumizi na biashara ya dawa hizo haramu.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE, CHACHA AKEMEA UZEMBE NA KUTOWAJIBIKA KWA BAADHI YA WATUMISHI WA SHULE YA WASICHANA TABORA

    June 10, 2025
  • MSAADA WA TREKTA KUTOKA SERIKALINI KUFUNGUA MILANGO YA KITIVO CHA KILIMO NA MAZINGIRA AMUCTA – MHE. CHACHA AONGOZA HAFLA YA MAKABIDHIANO.

    June 10, 2025
  • WATUHUMIWA 11 MBARONI KWA KUJIHUSISHA NA KILIMO CHA BANGI KATIKA ENEO LA HIFADHI YA MTO IGOMBE – TABORA.

    June 09, 2025
  • TABORA YAHITIMISHA MASHINDANO YA UMISSETA: MANISPAA YA TABORA YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA KATIKA MASHINDANO HAYO NGAZI YA MKOA

    June 06, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa