• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MKUU WA MKOA WA TABORA AONGOZA DUA MAALUM YA KULIOMBEA TAIFA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.

Posted on: October 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mheshimiwa Paulo Chacha, ameshiriki dua maalum ya kuliombea taifa kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025. Dua hiyo imeandaliwa na Kamati ya Amani ya Mkoa wa Tabora na kufanyika katika uwanja wa Shule ya Sekondari Uyui, ikihudhuriwa na waumini wa dini na madhehebu mbalimbali.

Akitoa salamu kwa niaba ya Kamati ya Amani ya Mkoa wa Tabora, Sheikh wa Mkoa wa Tabora, Ibrahimu Mavumbi, alisema lengo kuu la kusanyiko hilo ni kuonesha uzalendo na kuenzi amani na utulivu wa nchi.

“Uislamu unatambua kwamba uzalendo wa mwanadamu kuipenda nchi ni wajibu wake, pale ambapo kiongozi wetu mkubwa Mtume Mohamed (SAW) aliposema kwamba hakika alama ya Imani ya muislamu/muumini ni kuipenda nchi yake,” alisema Sheikh Mavumbi na kusisitiza kuwa ni jukumu la kila mmoja kuitetea na kuilinda amani ya taifa.

Kwa upande wake, Baba Askofu Muadhama Kardinali Protase Rugambwa, Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Tabora, aliishukuru Kamati ya Amani kwa kuwakutanisha watu wa dini na madhehebu mbalimbali kwa nia njema ya kuombea amani na utulivu wa taifa.

“Ndugu zangu, tuombee amani lakini tulifanye hilo sote kwa pamoja, tukishirikiana kwa pamoja bila unafiki, bila kujifanya kwa sababu muonekane hivi, na hakika kabisa tunaweza tukalipata na nchi yetu ikaendelea na tukawa bora katika amani hiyo ambayo tunaitafuta,” alifafanua Kardinali Rugambwa.

Akihutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kushiriki dua hiyo, Mheshimiwa Chacha aliipongeza Kamati ya Amani kwa uratibu mzuri wa tukio hilo na kuwahakikishia wananchi kuwa usalama upo wa kutosha kuelekea uchaguzi mkuu.

“Niwahakikishieni na niwape uhakika, amani ipo ya kutosha, laleni usingizi, fanyeni shughuli zenu kwa uhuru. Siku ya tarehe 29, ninyi nyote jitokezeni mkachague viongozi mnaowataka kuwaongozeni, bila hofu wala kuogopa. Hakuna mtu anayeweza kukudhuru, serikali ipo kwa ajili yenu,” alieleza Mheshimiwa Chacha.

Tukio hilo limebeba ujumbe wa mshikamano, upendo na uzalendo, likisisitiza dhamira ya mkoa wa Tabora kuendelea kuwa mfano wa amani, utulivu na umoja wa kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MKUU WA MKOA WA TABORA AONGOZA DUA MAALUM YA KULIOMBEA TAIFA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.

    October 24, 2025
  • TABORA YAENDELEA KUIMARISHA USIKILIZWAJI WA MASHAURI YA KESI KWA NJIA YA MTANDAO: MKUU WA MKOA AKABIDHI KOMPYUTA KWA JESHI LA MAGEREZA

    October 20, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZASOGEZWA KWA WANANCHI: MADAKTARI WABOBEZI 56 WAWASILI TABORA KUHUDUMIA WANANCHI

    September 29, 2025
  • MKOA WA TABORA WAONESHA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA ULINZI WA HAKI ZA MTOTO

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa