• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TABORA YAENDELEA KUIMARISHA USIKILIZWAJI WA MASHAURI YA KESI KWA NJIA YA MTANDAO: MKUU WA MKOA AKABIDHI KOMPYUTA KWA JESHI LA MAGEREZA

Posted on: October 20th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, amekabidhi jumla ya kompyuta 8 kwa Jeshi la Magereza mkoani humo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kuimarisha mfumo wa “Kesi Mtandao” unaolenga kurahisisha usikilizaji wa mashauri ya mahabusu na wafungwa bila usumbufu wa kusafiri mahakamani. Tukio hilo limefanyika leo katika Gereza Kuu la Uyui, mkoani Tabora.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Jaji Dkt. Adam Juma Mambi, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora, alisema Mahakama inaendelea kutekeleza mkakati wa matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa haki kwa kuzingatia dira ya maendeleo ya taifa. Alibainisha kuwa upatikanaji wa vifaa hivyo utasaidia kuongeza ufanisi katika usikilizaji wa mashauri bila wafungwa kuhudhuria moja kwa moja mahakamani.

“Kwa mwaka 2024/25 jumla ya mashauri 421 yamesikilizwa kwa njia ya mtandao, jambo ambalo limepunguza safari zisizo za lazima za kusafirisha wafungwa na watuhumiwa kwenda mahakamani, na hivyo kuongeza kasi ya utoaji haki kwa haraka na kwa wakati,” alisema Jaji Dkt. Mambi.

Katika hotuba yake baada ya kukabidhi vifaa hivyo pamoja na magodoro 168 kwa ajili ya wafungwa wa Gereza Kuu la Uyui, Mhe. Chacha aliwahimiza viongozi wa Mahakama na Magereza kutoshindwa kutekeleza majukumu yao kutokana na changamoto zinazoweza kuzuilika.

“Mhe. Jaji, sisi kama Serikali tupo bega kwa bega na vyombo vya utoaji haki. Usikumbane na changamoto yoyote ukakaa kimya. Ikiwa kuna jambo linalohitaji ushirikiano wa Serikali, nijulishe mapema ili tutatue changamoto hizo na kuruhusu kazi zenu ziendelee kwa ufanisi,” alisisitiza Mhe. Chacha.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Gereza Kuu la Uyui, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Musa Mkisi, aliishukuru Serikali kwa msaada wa vifaa vya TEHAMA na magodoro, akisema vitachangia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza mlundikano wa kesi na kuimarisha mazingira ya wafungwa.

Utekelezaji wa mfumo wa Kesi Mtandao mkoani Tabora unaendelea kuwa mfano bora wa matumizi ya teknolojia katika utoaji wa haki, sambamba na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha mifumo ya kidijitali katika taasisi za umma, kwa lengo la kuongeza uwazi, ufanisi, na upatikanaji wa haki kwa wakati.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABORA YAENDELEA KUIMARISHA USIKILIZWAJI WA MASHAURI YA KESI KWA NJIA YA MTANDAO: MKUU WA MKOA AKABIDHI KOMPYUTA KWA JESHI LA MAGEREZA

    October 20, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZASOGEZWA KWA WANANCHI: MADAKTARI WABOBEZI 56 WAWASILI TABORA KUHUDUMIA WANANCHI

    September 29, 2025
  • MKOA WA TABORA WAONESHA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA ULINZI WA HAKI ZA MTOTO

    September 26, 2025
  • RC CHACHA AFUNGUA KONGAMANO LA WAFANYABIASHARA WADOGO MKOA WA TABORA, AWASIHI WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA ZA ZABUNI ZA SERIKALI

    September 24, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa