• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

NENDENI MKATUMIE MAARIFA MLIYOYAPATA KUBORESHA UCHUMI WENU NA WA TAIFA – MHE. MAGEMBE.

Posted on: March 28th, 2025

Na. OMM - Tabora.


Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Cornel Lucas Magembe, amewataka wajasiriamali wa Mkoa wa Tabora kutumia maarifa waliyojifunza kuboresha uzalishaji wa bidhaa zao na kukuza uchumi wao pamoja na wa Taifa.

Akizungumza katika hafla ya kufunga mafunzo maalum ya ujasiriamali yaliyofanyika katika Nyumba ya Ujasiriamali Kitete, Mhe. Magembe alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha, na kusisitiza umuhimu wa kuyatumia mafunzo hayo kuboresha bidhaa ili ziweze kushindana katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Mafunzo hayo ya siku saba yaliandaliwa na kikundi cha ujasiriamali cha Grows Global Innovations Company Limited kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Tabora. Bi. Ashura Shabani Mwazembe, Mwenyekiti wa Grows Global Innovations, alisema kuwa lengo la mafunzo hayo lilikuwa ni kuwajengea uwezo wajasiriamali pamoja na wananchi wanaotamani kuingia katika sekta hiyo kwa kuwapatia maarifa juu ya utengenezaji wa sabuni za maji,sabuni za miche,marashi mbalimbali, usindikaji wa matunda na mbogamboga, ufugaji wa nyuki na usindikaji wa mazao ya nyuki, pamoja na mbinu za kuongeza thamani ya bidhaa katika soko.

Mafunzo hayo yaliendeshwa na mtaalamu mahiri wa ujasiriamali nchini, Dkt. Ladislaus Luambano (Baba wa Wajasiriamali) kutoka Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Meneja wa SIDO Mkoa wa Tabora, Bw. Samwel Neligwa, alikipongeza kikundi cha Grows Global Innovations kwa juhudi zao za kuandaa mafunzo haya, akisema kuwa yatawasaidia wajasiriamali kuinuka kiuwezo na kiuchumi, hivyo kuwawezesha kushindana katika masoko mbalimbali.

Akifunga rasmi mafunzo hayo, Mhe. Magembe alimpongeza Bi. Ashura Mwazembe kwa juhudi zake za kutafuta maarifa na ujuzi zaidi kwa ajili ya kuendeleza wajasiriamali wa Tabora. Aliwasihi wahitimu kutumia ujuzi waliopata si tu kwa manufaa yao binafsi, bali pia kwa maendeleo ya mkoa na taifa kwa ujumla.

Mafunzo haya yalifunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, na kufungwa na Mhe. Magembe kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa. Hafla hiyo ilihitimishwa kwa utoaji wa vyeti kwa wahitimu zaidi ya ishirini waliofanikiwa kuhitimu mafunzo hayo.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa