• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

NENDENI MKATUMIE MAGARI HAYA KWA KAZI ILIYOKUSUDIWA NA WALA SI KWA MATUMIZI MENGINEYO: MHE. CHACHA.

Posted on: February 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha, ameongoza zoezi la makabidhiano ya magari mawili mapya kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Jamii Salama, unaofadhiliwa na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete. Zoezi hilo limefanyika nje ya ukumbi wa mikutano wa Isike Mwanakiyungi mkoani Tabora.                     

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete, Bi. Vanessa Anyoti, alisema wilaya za Sikonge na Uyui zimechaguliwa kama sehemu za majaribio kwa ajili ya utoaji wa  huduma za kliniki tembezi. Bi. Anyoti alieleza kuwa mradi huu utatoa uzoefu muhimu kwa wilaya na mikoa mingine nchini, na kuimarisha huduma za afya katika maeneo mengine.

Mradi wa Jamii Salama, unaotekelezwa katika wilaya hizi mbili, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto nchini. Awamu ya kwanza ya mradi huu itahusisha utoaji wa huduma za kliniki tembezi,ujenzi wa zahanati mbili, Gengesita katika wilaya ya Uyui na Ipembe katika wilaya ya Sikonge, huku mkoa wa Tabora ukitumika kama mfano wa utekelezaji wa mradi huu.

Mhe. Chacha aliwataka viongozi wa wilaya hizi mbili kutumia magari hayo kwa malengo yaliyokusudiwa, akisisitiza kuwa ni muhimu kuhakikisha matumizi bora ya vifaa hivyo kwa kuvitunza na kuvifanyia ukarabati kwa wakati. Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora, Ndg. Said Nkumba, alishukuru kwa kuanzishwa kwa mradi huo mkoani Tabora, akitaja kuwa huduma za afya zimeimarika sana, na mabadiliko ya utoaji huduma yameonekana wazi.

Kwa upande wao, wenyeviti wa Halmashauri za Sikonge na Uyui walitoa shukrani kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwaletea mradi huo, wakisema utasaidia kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wao.

 Mbali na makabidhiano ya magari kwa ajili ya mradi wa Jamii Salama, Mhe. Chacha alikabidhi pia gari moja aina ya Isuzu kwa Katibu Tawala wa mkoa wa Tabora,Dkt. John Mboya, kwa ajili ya usambazaji wa chanjo katika mkoa wa Tabora. Aidha, alikabidhi magari matatu aina ya Ford kwa wakuu wa wilaya za Uyui, Nzega, na Urambo, ili kusaidia utoaji wa huduma bora za serikali katika maeneo yao.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa