Leo Oktoba 25, 2023 Benki ya NMB imemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Batilda Salha Burian Hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni 374.3 ikiwa ni fidia kwa Wakulima wa Tumbaku 1398 waliokumbwa na janga la Mvua za mawe zilizopata kunyesha mwanzoni mwa mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwasili katika Ukumbi wa Isike Mwanakiyungi kuhudhuria hafla ya kukabidhi Hundi ya fidia kwa Wakulima wa Tumbaku walioathirika na mvua za mawe
Baadhi ya viongozi wa Serikali, wawakilishi kutoka vyama vya Msingi (AMCOS) Mkoani Tabora pamoja na wadau wa sekta ya kilimo wakiwa ndani ya Ukumbi wa Isike Mwanakiyungi kushuhudia hafla ya kukabidhi Hundi ya fidia kwa Wakulima wa Tumbaku walioathirika na mvua za mawe.
Kwa niaba ya Wakulima wa Tumbaku Mkoani Tabora Ndugu, Deoglatias Paulo Mwenyekiti (AMCOS) Mtapenda akitoa neno la Shukrani kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian na Watendaji wa Benk ya NMB, wakati wa hafla ya kukabidhi Hundi ya fidia kwa Wakulima wa Tumbaku walioathirika na mvua za mawe. Oktoba 25,2023
Dkt. Lupilya Emmy Meneja wa Mamlaka ya Bima Tanzania kanda ya Magharibi akitoa salamu kutoka Benki ya NMB kanda ya Magharibi wakati wa hafla ya kukabidhi Hundi ya fidia kwa Wakulima wa Tumbaku walioathirika na mvua za mawe. Oktoba 25, 2023.
Katika salamu zake amemuhakikisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, Benki ya NMB itaendelea kutoa elimu ya Bima ya Mazao kwa wakulima wa Tumbaku ili kuhakikisha Wakulima wa tumbaku wanakabiliana na majanga ya mvua za mawe.
Ndugu Nsolo Mlozi Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa Benki ya NMB amesema kuwa, maboresho ya miundombinu ya barabara yaliofanywa na Serikali ya Dkt. Samia, Mkoani Tabora yamewavutia Watendaji wa Benki ya NMB kuwekeza fedha nyingi Mkoani humo hususani kwenye Sekta ya Kilimo (Tumbaku) ambacho kimekuwa na mchango mkubwa kwenye uchumi wa taifa. Na tayari Benki ya NMB imeunda kitengo maalumu kitakacho husika na kilimo cha tumbaku peke yake.
Akitoa salamu zake, Ndugu Nsolo Mlozi ameeleza mchango mkubwa wa Serikali ya Awamu ya sita kwa kuhimarisha miundombinu ya barabara ambayo imerahisisha shughuli nyingi za kiuchumi na kilimo kikiwemo. Lakini pia Ndugu Nsolo ameihakikishia Serikali kuwa, Benki ya NMB itahakikisha inashirikiana na wakulima wa Tumbaku hususani katika suala la utolewaji wa elimu ya bima ya mazao.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akihutubia watendaji wa Benki ya NMB pamoja na Wawakilishi kutoka Vyama Vya Msingi vinavyojumuhisha wakulima wa Tumbaku Mkoani Tabora kwenye hafla ya kukabidhi Hundi ya fidia kwa Wakulima wa Tumbaku walioathirika na mvua za mawe iliyofanyka katika Ukumbi wa Isike Mwana Kiyungi, Oktoba 25, 2023.
Sehemu kubwa ya hotuba yake, Dkt. Batilda Burian amemshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapa nafasi wadau mbalimbali kuwekeza kwa wakulima hususani suala la Bima ya Mazao. Sambamba na utengaji wa fedha kwa ajili ya Ruzuku ya mbolea. Pia amewashukuru na kuwapongeza watendaji wote wa Benki ya NMB kwa kusimamia maslahi ya wakulima wa Tumbaku hususani kipindi cha mvua ya Mawe kwa kutoa fidia ya Shilingi Milioni 374.3 na kunufaishi wakulima 1398.
Na pia alitoa wito kwa wakulima wa tumbaku Mkoani Tabora kuchanamkia fursa ya Bima ya Mazao ili kupambana na majanga ya asili hasa mvua za mawe ambazo huaribu zao la tumbaku kwa kiasi kikubwa sana.
Kwa niaba ya Wakulima wa Tumbaku, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amepokea Hundi ya Shilingi Milioni 374.3 kutoka Benki ya NMB kama sehemu ya fidia kwa Wakulima 1398 walioathiriwa na mvua za mawe.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akimkabidhi Hundi ya Shilingi Milioni 374.3 Ndugu, Deoglatias Paulo Mwenyekiti (AMCOS) Mtapenda kwa niaba ya Wakulima 1398 walioathiriwa na mvua za mawe.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji kutoka Benki ya NMB mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kukabidhi Hundi ya fidia kwa Wakulima wa Tumbaku walioathirika na mvua za mawe iliyofanyika leo Oktoba, 25 2023 kwenye Ukumbi wa Isike Mwanakiyungi.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa