• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC AAGIZA HADI MWISHONI MWA SEPTEMBA HOSPITALI YA WILAYA SIKONGE ITOE HUDUMA MATIBABU ZAIDI

Posted on: August 17th, 2020

RC  AAGIZA HADI MWISHONI MWA SEPTEMBA HOSPITALI YA WILAYA SIKONGE ITOE HUDUMA MATIBABU ZAIDI

UONGOZI wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge kuhakikisha ifikapo mwisho wa Septemba mwaka huu wanaongeza huduma mbalimbali za matibabu katika Hospitali hiyo.

Agizo hilo limetolewa  na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Philemon wakati muendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye maeneo mbalimbali wilayani Sikonge.

Dkt. Sengati alisema ni lazima watoe fedha za kuwalipa mafundi ili waweze kukamilisha shughuli ndogo zilizobaki na hatimaye waweze kuweka vifaa ambayo vitawezesha kupanua wigo wa matibabu kwa wananchi.

Alisema Hospitali teule inayotumika hivi sasa imeshaelemewa kutokana kuwa ilijengwa miaka mingi wakati idadi wa wakazi wa Sikonge ilikuwa ndogo na hivi sasa wameongeza na hivyo kuwalizimu kutaka kupata huduma za matibabu katika hospitali hiyo kubwa.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge ambao hawana bima kujiunga na na Mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa ICHF ili kuweza kupata matibabu kutoka ngazi za Zahanati hadi Hospitali za Rufaa za Mikoa kwa kutumia gharama za shilingi 30,000/- kwa mwaka.

Alisema haua hiyo itawasaidia kuwa na uhakika wa kupata huduma za matibabu kwa watu sita wa kaya moja.

Dkt. Sengati alisema wananchi wakiwa na afya bora wataweza kushiriki kikamilifu katika katika shughuli za kujiletea maendeleo yao na ujenzi wa uchumi wa nchi kwa ujumla.

Aidha aliwataka wataalamu kuendelea kutoa elimu ili wananchi wengi waweze kujiunga na ICHF iliyoboreshwa.

 

 Mwisho

RC ATAKA SIKONGE KUTENGA ENEO KUBWA LA UWEKEZAJI

MKUU wa Mkoa wa Tabora Dkt. Philemon Sengati ameitaka Halmashauri ya Wilya ya Sikonge kutenga maeneo makubwa na ambayo hayana migogoro kwa ajili ya uwekezaji mkubwa na mdogo.

Alitoa kauli hiyo mara baada ya kutembelea eneo ambalo Halmashauri hiyo inakusudia kujenga Kiwanda cha kuchakata na kufungasha mazao ya nyuki wakati muendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye maeneo mbalimbali wilayani Sikonge.

Alisema ni lazima wawe na mpango wa muda mrefu kutafuta eneo kubwa lililopimwa na ambalo halina migogoro ili Mkoa uwasaidia kuwatafutia wawekezaji mbalimbali ambao watasaidia kujenga viwanda ambavyo vitasaidia kuiendeleza wilaya na Mkoa kwa ujumla.

“Mtafute maeneo ambayo hata mwekezaji akija hawezi kukutana na watu kuvamilia eneo lake na wakati mwingine kuharibu mali zake” alisema.

Alisema kuwa Hekta nne walizotenga hazitoshi pindi wawekezaji wakubwa wakitokeza kutaka kuwekeza, hivyo ni vema wakaongeza eneo ili kupata eneo kubwa la uwekezaji.

Dkt.Sengati alisema uongozi wa Mkoa unaendelea na jitihada za kutafuta wawekezaji wa ndani na nje ya Nchi ili kuwavutia wawekezaji kwa ajili ya kujenga viwanda ambavyo vitasaidia kuupandisha kiuchumi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Peres Magiri alisema wamepanga kuongeza eneo na kufikisha  Hekta 500 kwa ajili ya uwekezaji.

Alisema juhudi mbalimbali zinaendelea za kuyaanisha kwa ajili ya kulipa fidia wamiliki wake.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Gadi Mwatebela alisema baada ya andiko la mradi kupitia ,Mfuko wa Mistu Tanzania umetoa udhibitisho wa fedha za ujenzi wa kiwanda cha kuchakata na kufungasha mazao ya nyuki.

Alisema Kiwanda hicho kitagharimu shilingi milioni 757.5 ambapo Mfuko wa Mistu Tanzania unatarajia kutoa milioni 719.7 na Halmashauri itachangia shilingi milioni 37.8

 

mwisho

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa