RC KUWA MGENI RASMI KWENYE MCHEZO WA NUSU FAINALI KATI BIASHARA NA YANGA
MKUU wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani anatarajiwa kuwa Ngeni rasmi kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya michuano ya kombe la Shirikisho baina ya Biashara United ya Mara dhidi ya Yanga ya Jijini Dar es salaam.
Mchezo huo utachezwa mchana katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.
Msindi wa mchezo huo atasubiri mshini kati ya Simba na Azam ambazo zinatarajiwa kucheza siku ya Jumamosi katika Uwanja wa Maji maji mjini Songea.
Akizungumza na waandishi wa habari Kocha wa magolikipa wa Yanga Razak Siwa alisema wachezaji wake wako katika hali nzuri na wanatarajia kuondoka na ushindi.
Alisema lengo lao ni kushinda kila mechi iliyopo mbele yao ikiwemo ya kwao na Biashara United katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.
Kwa upande wa Kocha wa Biashara United ya Mara Omary Hamis alisema wako tayari kwa mchezo wa kesho kwa kuwa lengo lao ni kufika fainali na kutaa ubingwa ili waweze kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.
Meneja Masoko wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF )Aaron Nyanda alisema maandalizi ya mchezo yamekamilika ambapo timu zote zimefika na waamuzi wa mchezo huo tayari wameshafika.
Alisema kuwa lengo la kupeleka michezo hiyo katika maeneo mbalimbali ni kuhamasisha mchezo huo na kukuza ushirikiano na biashara.
Nyanda alivitaja viingilio vya mchezo huo kuwa vitakuwa mzunguko shilingi 5,000/- na VIP ni shilingi 10,000/=
Mwisho
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa