• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC TABORA AAGIZA TARI –TUMBI KUZALISHA MBEGU BORA ZA ALIZETI

Posted on: July 26th, 2021

Na  Tiganya Vincent

RS-Tabora

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani  amewaagiza Watafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi cha Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI) kuhakikisha wanazalisha mbegu bora za Alizeti zitakazowawezesha wakulima kulima na kupata mavuno mengi.

Hatua hiyo inalenga kuongeza uzalisha wa alizeti kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la upatikanaji wa mafuta hapa nchini.

Balozi Dkt. Batilda alitoa agizo hilo leo wakati akipokuwa na ziara ya kikazi katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi cha Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI)

Amesema Nchi inakabiliwa na upungufu mafuta karibu tani laki nne na hivyo jitihada zinahitajika kusaidia kubaini maeneo ambayo yanafaa kwa uzalishaji wa alizeti ili wakulima wapatiwe mbegu bora ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

Balozi Dkt. Batilda amesema hatua itasaidia kujua ni ekari ngapi mkoani Tabora zinafaa kwa alizeti na mahitaji halisi ya mbegu bora kwa mashamba yote.

Ameongeza hali hiyo itasaidia kujua Maafisa Ugani wangapi wanahitaji kwa ajili ya kuwasaidia wakulima kuzalisha kwa ubora na wingi wa zao hilo.

Balozi Dkt. Batilda amesema katika kuhakikisha hilo lifanikiwa ameitisha kikao cha Halmashauri zote na Taasisi zote za Utafiti na wadau wiki ijayo kwa lengo la kupanga mikakati ya kufanikisha zoezi hilo.

Katika Hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora amewapongeza Watafiti wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo –Tumbi cha Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI) kwa kuweza kuzalisha mbegu ya mahindi ambayo umesaidia kuongeza uzalishaji wa mahindi kwa ekari moja hadi kufikia magunia 22.

Amesema hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha wananachi wanakuwa na mbegu zitakazowawezesha kuwa na uhakika wa kupata chakula cha kutosha mwaka mzima.

Balozi Dkt. Batilda amewataka Watafiti hao kuongeza pia juhudi katika uzalishaji wa mbegu za viazi lishe na kuzisambaza kwa wananchi ili watu wengi waweze kulima kwa ajili ya kukabiliana na tatizo wa utapia mlo.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Tabora amezitaka kaya tisa zilizovamilia eneo la TARI –Tumbi kuondoka ili waweze kuendelea na shughuli zao za utafiti kwa maslahi mapana ya Nchi.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa