• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC TABORA AKABIDHI MAGARI SITA KWA WAKUU WA WILAYA YA JESHI LA POLISI

Posted on: November 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amekabidhi magari manne ya Kubeba Wagonjwa kwa Wakuu wa Wilaya ya Kaliua, Sikonge na Uyui, ikiwa ni moja ya kumalisha usambazaji wa magari ya wagonjwa 900 yenye thamani zaidi ya Shilingi Bilioni 29, yaliotolewa kwa Halmashauri zote hapa nchini kwa malengo ya kukuza huduma za Afya hasa huduma ya Mama na Mtoto. Na magari mawili ya jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora  yaliotolewa kwa malengo ya kukuza suala la ulinzi Mkoani Tabora.

Akikabidhi magari Hayo manne kwa halmashauri ya Sikonge, Kaliua na Uyui na magari mawili kwa ajili ya jeshi la Polisi, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wasimamizi wa magari hayo kuhakikisha magari hayo yanatumika katika matumizi yaliopangwa na si matumizi mengine kama kubeba madawa ya kulevya na vitu vingine visivyohitajika.

Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Sikonge na Kaliua Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Zakalia Mwansasu akitoa neno la shukrani kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za kinunulia magari ya Wagonjwa manne, ambapo leo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian ameyakabidhi kwa wakuu hao wa Wilaya.

Akitoa neno la Shukrani, Mhe. Zakalia Mwansasu amehaidi kuyatunza na kuyalinda magari ya kubebea wagonjwa ili kuhakikisha thamani ya Fedha zilizotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia zinafanya kazi ipasavyo kwa maslahi ya watanzania.

Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC), Ndugu Hassan Wakasuvi, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa kupitia Mkoa wa Tabora Mohamed Nassoro Hamdan akitoa salamu za Chama cha Mapinduzi  wakati wa hafla ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora kukabidhi magari manne ya kubeba Wagonjwa kwa Wakuu wa Wilaya ya Sikonge, Uyui na Kaliua iloyofanyika katika Ukumbi wa Isike Mwanakiyungi. Novemba 16, 2023.

Akitoa salamu za chama Ndugu. Mohamed Nassoro ameeleza kuwa, kama viongozi wa chama hawana budi kumshukuru Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inatekelezwa kikamilivu kwa hapa Mkoani Tabora na Tanzania kwa ujumla. Na kusema kuwa kupitia haya yanafanywa na Mhe. Rais yanatufanya sisi viongozi na wanachama kutembea kifua mbele.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akimkabidhi Magari mawili ya Polisi Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora Kamishina Msaidizi wa Polisi Richard Abwao. 

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Zakalia Mwansasu funguo mbili  za magari ya Kubeba Wagonjwa.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akimkabidhi ufunguo wa Gari la Kubeba Wagonjwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Mhe. Rafael Lufungija aliyeambata na Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Mhe. Dkt. Rashidi Chuachua.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Wilaya, Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Baadhi ya watumishi kutoka Ofiisi ya Mkuu wa Mkoa na Wilaya na wadau wa sekta ya afya walioshiriki kwenye hafla ya kukabidhi magari manne ya kubeba wagonjwa na magaro mawili ya jeshi la polisi.

Hafla ya kukabidhi magari manne ya  kubeba wagonjwa na magari mawili ya Jeshi la Polisi imefanyika katika Ukumbi wa Isike Mwanakiyungi na kuhidhuriwa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, wadau wa sekta ya Afya pamoja na watendaji kutoka ngazi ya Mkoa na Wilaya.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa