Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amekabidhi magodoro zaidi ya mia mbili (200) na Mablanketi kwa wanafunzi 210 wa shule ya sekondari Ziba waliounguliwa na vitu vyao kufuatia ajali ya kuungua moto bweni la wavulana iliyotokea asubuhi ya Januari 23, 2024.
“Tulipokea taarifa hizi kwa masikitiko sana kufuatia kuungua kwa bweni hilo, na tunamshukuru Mungu hakuna madhara yoyote ya kibinadamu yaliotokea, na sisi kama viongozi tumeona ni busara kufika usiku na kuwapatia magodoro na mablanketi haya ili muweze kulala kwenye mazingira mazuri angalau” alisema Mkuu wa Mkoa.
Ameongeza kuwa, wadau mbalimbali wamejitokeza kutoa misaada ya kibidamu kuhakikisha wanafunzi hao wanapatiwa msaada huku serikali ikiangalia hatua zingine.
“kwa sasa tunaweza kufanya ukarabati bwalo liliopo hapa ili liweze kutumika kama sehemu ya kulala kwa wanafunzi hawa, wakati serikali ikiangalia hatua zingine za kujenga bweni lingine”aliongeza Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa.
Aidha mkuu wa Mkoa ametoa pongezi kwa viongozi wa serikali na vyombo vya ulinzi ngazi ya mkoa na wilaya ambavyo vimefanya kazi kutwa nzima kuhakikisha wanafunzi hawa wanapatiwa msaada wa awali.
Bweni moja la wanafunzi wa shule ya sekondari Ziba wilayani Igunga limeteketea kwa moto asubuhi ya Jumanne Januari 23, 2024 huku chanzo cha moto huo kikiwa hakijulikani
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa