Na Tiganya Vincent
RS-Tabora
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani amewashukuru washabiki wa Timu za Simba na Yanga kwa kutumia usafiri wa Treni kwenda mchezo wa fainali ambao ulipigwa katika dimba la Tanganyika Mkoani Kigoma.
Amesema hatua imesaidia kuonyesha kuwa makundi makubwa ya wasafiri wanaweza kutumia usafiri wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) kusafiri katika maeneo mbalimbali.Balozi Dkt. Batilda amesema hayo leo baada ya kukutana na wasanii na washabiki wa timu ya Simba na Yanga waliokuwa wakitokea Kigoma.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amesema kufuatia michezo kuwa muhimu katika kutengeneza ajira kwa vijana na kuongeza kipato kwa wakazi wameamua kuweka mikakati ya kuhakikisha timu ya Rhino Rangers inapanda Ligi Kuu.
Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Buriani ametoa wito kwa washabiki wa Simba na Yanga na wadau wengine kujitokeza kwa wingi kuwekeza Mkoani huo katika sekta mbalimbali.
Amesema kuwa yapo maeneo mbalimbali ya uwekezaji ikiwemo ardhi kwa ajili ya kilimo cha mazao tofauti tofauti na utalii.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa