• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI YAJIPANGA KUIMARISHA HUDUMA ZA UGONJWA WA SIKO SELI NCHINI.

Posted on: June 19th, 2025

Na. OMM Tabora.

Serikali kupitia Wizara ya Afya imejipanga kuhakikisha kuwa hospitali zote na vituo vyote vya  afya nchini vinakuwa na kliniki za kutolea huduma kwa wagonjwa wa siko seli (seli mundu), ili kuwafikia wagonjwa wengi zaidi kwa wakati.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Benedict Komba, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Siko Seli Duniani yaliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete. Dkt. Benedict amesema hatua hiyo inalenga kuimarisha mazingira rafiki ya utoaji wa huduma, na ametoa wito kwa wananchi kushirikiana na serikali kwa kuwapeleka watoto hospitalini mara tu wanapobainika kuwa na viashiria vya ugonjwa huo.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete, Dkt. Joachim Eyembe, amesema hospitali hiyo imeweka utaratibu wa kuwapima watoto wachanga ili kubaini mapema ugonjwa huo. Amesisitiza kuwa huduma za kliniki kwa wagonjwa zitaendelea kutolewa pamoja na ushauri nasaha kwa familia na jamii kwa ujumla.

Takwimu zinaonesha kuwa hadi sasa, Tanzania ina zaidi ya wagonjwa wa siko seli 14,000 waliogunduliwa, ambapo zaidi ya wagonjwa 8,000 wanatokea mkoani Tabora pekee. Ugonjwa huu wa kurithi kutoka kwa wazazi kwenda kwa watoto unaendelea kuwa changamoto inayohitaji hatua za haraka na madhubuti.

Maadhimisho ya Siku ya Siko Seli huadhimishwa kila mwaka ifikapo Juni 19, na kwa mwaka huu yameongozwa na kaulimbiu isemayo: "Hatua Madhubuti za Kitaifa kwa Matokeo Chanya ya Kijamii; Kuwezesha Jamii Kutambua, Kuzuia na Kukabiliana na Siko Seli."

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SERIKALI YAJIPANGA KUIMARISHA HUDUMA ZA UGONJWA WA SIKO SELI NCHINI.

    June 19, 2025
  • “TUSIRUHUSU KIWANGO CHA ADHABU KISICHO NA KIASI KWA MTOTO – MHE.TUKAI AONYA

    June 16, 2025
  • MHE, CHACHA AKEMEA UZEMBE NA KUTOWAJIBIKA KWA BAADHI YA WATUMISHI WA SHULE YA WASICHANA TABORA

    June 10, 2025
  • MSAADA WA TREKTA KUTOKA SERIKALINI KUFUNGUA MILANGO YA KITIVO CHA KILIMO NA MAZINGIRA AMUCTA – MHE. CHACHA AONGOZA HAFLA YA MAKABIDHIANO.

    June 10, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa