• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI YATOA SHILINGI BILIONI 26.9 KUWAINUA WAKULIMA KUPITIA MRADI WA UMWAGILIAJI MWAMAPULI – IGUNGA

Posted on: June 3rd, 2025

Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imezindua rasmi utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Scheme ya Umwagiliaji ya Mwamapuli iliyopo Kijiji cha Mwanzugi katika Kata ya Igunga, Wilaya ya Igunga, mkoani Tabora. Mradi huu unalenga kuongeza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 630 hadi kufikia hekta 2,397, sawa na ekari 5,923, ambapo wakulima zaidi ya 2,470 wanatarajiwa kunufaika moja kwa moja na mradi huo.

Akisoma taarifa ya mradi huo, Mhandisi wa Umwagiliaji wa Mkoa wa Tabora,Francis Mgangaluwa, alisema kuwa mradi huu unakusudia kuongeza tija katika kilimo cha umwagiliaji kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao na kipato kwa wakulima wa eneo hilo. Aidha, mradi huu utasaidia kuongeza usalama wa chakula katika Mkoa wa Tabora na nchi kwa ujumla.

Utekelezaji wa mradi huu utafanywa na Mkandarasi mzawa, kampuni ya Salum Motors Transport (SAMOTA) kutoka Nzega, chini ya usimamizi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji. Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 7 Machi 2025, na kazi zinatarajiwa kuanza rasmi tarehe 10 Juni 2025. Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha siku 720, ambapo thamani yake ni shilingi bilioni 26.9.

Kazi zitakazofanyika katika mradi huu ni pamoja na ujenzi wa barabara za mashambani zenye urefu wa kilomita 28 kwa kiwango cha changarawe, ujenzi wa mifereji ya matupio yenye urefu wa kilomita 27, pamoja na ujenzi wa mitalo ya zenge, vigawa maji, box karavati saba na pipe karavati. Pia kutajengwa ofisi ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, nyumba ya Meneja wa Scheme pamoja na ununuzi wa  gari moja kwa ajili ya usimamizi wa mradi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, aliwapongeza wakulima wa Igunga kwa ushirikiano wao mkubwa kwa Tume ya Umwagiliaji na uongozi wa Wilaya ya Igunga katika maandalizi ya mradi huu. Aidha, alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 26 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo muhimu wa maendeleo. Dkt. Mboya alitoa wito kwa Mkandarasi kuhakikisha anatekeleza mradi kwa ubora wa hali ya juu na kwa wakati uliopangwa, akisisitiza kuwa viongozi wa mkoa watakuwa karibu katika kusimamia kila hatua ya utekelezaji.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mboya alionesha kusikitishwa na mila na desturi zinazokwamisha maendeleo ya wananchi wa kijiji cha Chumachankola, waliopinga utekelezaji wa mradi kwa madai kuwa eneo hilo hutumika kwa ajili ya matambiko. Alitoa wito kwa wananchi kubadilika kifikra na kuendana na maendeleo ya karne ya sayansi na teknolojia, akisema ni wakati wa kuachana na mila zinazokwamisha juhudi za Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Mhe. Sauda Mtondoo, alieleza kuwa mradi huo ni uti wa mgongo wa uchumi wa wananchi wa Igunga, kwani unaleta uhakika wa uzalishaji wa chakula bila kutegemea mvua. Alisisitiza kuwa Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kwa dhati kuinua uchumi wa wananchi kupitia uwekezaji mkubwa katika sekta ya umwagiliaji.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, akihutubia wananchi waliohudhuria hafla ya kukabidhi rasmi mradi  huo kwa Mkandarasi, aliwashukuru wananchi wa Igunga kwa kuupokea mradi kwa moyo wa uzalendo na ushirikiano. Hata hivyo, alilaani vikali kitendo cha baadhi ya wananchi wa kijiji cha Chumachankola kupinga mradi kwa sababu ya kulinda eneo la matambiko. Aliahidi kuwa Serikali ya Mkoa italifanyia kazi suala hilo kwa busara na hekima ili kupata suluhu ya kudumu. Mhe. Chacha pia aliwakumbusha wanachama wa scheme hiyo kuhakikisha wanalipa ada zao kwa wakati na kwa uaminifu, huku akisisitiza umuhimu wa viongozi wa scheme kuwa na uwazi katika usomaji wa mapato na matumizi kwa wanachama wao.

Katika hatua nyingine ya hotuba yake, Mhe. Chacha alikemea vikali kitendo cha raia mmoja kuchana kitambulisho cha Afisa wa TAKUKURU aliyekwenda kutekeleza wajibu wake kwa mtuhumiwa, akisema kuwa Serikali haitavumilia tabia ya wananchi kuchukua sheria mkononi au kupambana na watumishi wa umma walioko kazini. Alitoa onyo kali kwa yeyote atakayejaribu kuzuia au kuvuruga utekelezaji wa sheria za nchi.

Viongozi wa Wilaya ya Igunga kwa pamoja waliahidi kushirikiana kikamilifu kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa wakati, kwa ubora na unatunzwa ipasavyo kwa manufaa ya wananchi wote wa Igunga na Mkoa wa Tabora kwa ujumla.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI WILAYANI URAMBO: KWA KUFANYA USAFI, KUPANDA MITI NA KUTOA WITO WA KUTUNZA MAZINGIRA.

    June 05, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI - JUNI 5, 2025.

    June 04, 2025
  • SERIKALI YATOA SHILINGI BILIONI 26.9 KUWAINUA WAKULIMA KUPITIA MRADI WA UMWAGILIAJI MWAMAPULI – IGUNGA

    June 03, 2025
  • KAMANDA ABWAO AFUNGUA RASMI UMISSETA TABORA, AHIMIZA NIDHAMU NA UZALENDO KWA WANAMICHEZO.

    June 02, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa