• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TAASISI ZA UMMA MKOANI TABORA ZINADAIWA ZAIDI YA BILIONI 1.8 ZA BILI ZA MAJI

Posted on: August 25th, 2020

TAASISI ZA UMMA MKOANI TABORA ZINADAIWA ZAIDI YA BILIONI 1.8 ZA BILI ZA MAJI

MAMLAKA tatu za Maji safi na Usafi wa Mazingira Mkoani Tabora zinadaia taasisi mbalimbali za umma bili ya huduma ya maji ya zaidi ya shilingi bilioni 1.8.

Kauli hiyo imetolewa na Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Maji za Tabora , Nzega na Igunga wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt Philemon Sengati ya kukagua mradi wa kutoa maji ziwa Victoria kwenda Mkoani humo.

Mkurugenzi  Mtendaji wa TUWASA Joel Rugemalila alisema kwa uapnde wao wanazidai Taasisi za Umma kiasi cha shilingi bilioni 1.7 ikiwa ni malimbikio ya madai ya madeni ya bili za maji za mwaka wa fedha wa 2017/18, 2018/19 na  2019/20.

Alisema miongoni mwa wadai ni pamoja na Jeshi, Magereza , Polisi na Hospitali

Rugemalila alisema makusanyo halisi ya TUWASA kwa mwezi yatakiwa kuwa zaidi ya shilingi milioni 450 lakini kutokana na Taasisi hizo kutolipwa kwa madeni ya maji wamekuwa wakishuka katika ukusanyaji na kupata kiasi cha milioni 350 kwa mwezi.

Alisema hali hiyoimesababisha kuwepo ugumu wa uendshaji wa Mamlaka hiyo kwa kuwa inahitaji shilingi milioni 90 za umeme na shilingi milioni 60 za kununulia dawa za kusafisha maji.

Mkurugenzi huyo Mtendaji wa UWASA aliongeza kuwa wamekuwa wakitoa kiasi cha milioni 145, kulipa mishahara ya watumishi na shilingi milioni 64 kulipa Mamlaka ya Maji ya Kahama Shinyanga (KASHUWASA) ikiwa ni malipo ya maji wanayonunua kutoka kwao ili kuwasambazia wateja.

Rugemalila alisema wangekuwa wakilipwa fedha hizo zingesaidia sana kuboresha huduma za upatikanaji wa maji kwa wananchi kwa wakati kwa kuongeza mitandao ya maji katika maeneo yote ambayo hayajafikiwa.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamalaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Mji wa Nzega Lightness Gai alisema wanadai Taasisi mbalimbali za Serikali jumla ya shilingi milioni 43.9.

Alisema wamekuwa wakifuailia lakini kasi ya ulipaji umekuwa mdogo jambo ambalo limesababisha kupungukiwa fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya zamani ya kusafirishia maji.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Igunga (IGUWASA) Athuman Kiludumya alisema wanadai Taasisi za umma zaidi ya shilingi milioni 56.1.

Alisema Taasisi wanazidai ni Magereza, Polisi na Hospitali ya Wilaya.

Kufuatia hali, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Sengati ameziagiza Mamlaka zote tatu za utoaji wa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kuhakikisha zinampelekea orodha ya wadaiwa na kiasi ili aweze kukutana nazo.

Alisema anataka kukutana nazo ili ziweze kuonyesha mpango wao wa kulipa madeni yao ili fedha zitakazopatikana ziweze kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wale wote ambao hawajafikiwa na huduma hiyo.

Mwisho

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa