Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amebainisha mipango ya mkoa wa Tabora kujenga kiwanda cha kuzalisha mizinga ya nyuki ili kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki mkoani humo. Ameyasema hayo alipokuwa akihutubia kwenye mdaharo wa sekta binafsi na sekta za umma wenye malengo ya Kuhamasisha ushiriki wa sekta binafsi katika uhifadhi wa shoroba kupitia uwekezaji endelevu wenye tija kwa serikali na makundi mbalimbali katika jami, uliofanyika katika Ukumbi wa hotel ya JB Serries Februari 27, 2024
Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema kuwa, Mkoa wa Tabora umebarikiwa kuwa na mazao ya nyuki ambayo yamekuwa na tija kwa wakazi wa mkoa wa Tabora, na hivyo kama serikali ina wajibu wa kuhakikisha kunawekwa mikakati ya kujenga kiwanda cha kutengeneza mizinga ya nyuki ili kukuza uzalishaji wa mazao ya nyuki.
Aidha, Dkt. Batilda ameipongeza Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa kuchagua mkoa wa Tabora kuwa miongoni mwa mikoa ambayo inafaidika na mradi wa USAID Tuhifadhi Maliasili kwa kuona umuhimu wa kushirikiana na serikali katika kuhamasisha ushirikishwaji wa wadau katika kuhamasha shughuli endelevu za kiuchumi ndani ya maeneo ambako shughuli za binadamu na Wanyama pori huingiliana. Na kutoa wito kwa Taasisi hiyo kupitia wanachama wake TCCIA na TWCC kuwa mabalozi wa kutangaza bidhaa bora za Tanzania, hasa bidhaa zinazozalishwa mkoani Tabora.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa