• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TABORA YAZINDUA RASMI MRADI WA YEFFA KUWAWEZESHA VIJANA KIUCHUMI.

Posted on: January 29th, 2026

Akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji, Ndg. Dietrich Mwinuka, ameongoza kikao cha utambulisho wa Mradi wa YEFFA (Youth Entrepreneurship for the Future of Food and Agriculture) unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania Agricultural Modernization Association (TAMA) na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

Awali akiwasilisha maelezo ya mradi huo, Afisa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka TAMA, Ndg. Frank Shinge, amesema kuwa mradi wa YEFFA unalenga kuwajengea uwezo vijana kupitia mafunzo ya ufundi stadi katika maeneo ya uendeshaji na matengenezo ya mitambo ya kilimo (agro-mechanization), mifumo ya umwagiliaji pamoja na usindikaji wa mazao. Ameongeza kuwa mradi huo unafadhiliwa na Shirika la AGRA, na utekelezaji wake umeanza rasmi mwezi Novemba 2025 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2027.

Ndg. Shinge amesema kuwa mradi huo unatekelezwa katika mikoa minne ya Kanda ya Kati ambayo ni Tabora, Manyara, Singida na Dodoma, na unatarajia kuwawezesha jumla ya vijana 1,525 kwa kuwapatia mafunzo ya moja kwa moja katika ujuzi wa umechanishaji wa kilimo, ikiwemo uendeshaji na matengenezo ya mitambo ya kilimo, umwagiliaji pamoja na usindikaji wa mazao.

Ameeleza kuwa, katika utekelezaji wake, mradi wa YEFFA umeweka mkazo mkubwa katika usawa wa kijinsia ambapo asilimia 70 ya wanufaika wanatarajiwa kuwa wanawake, kwa lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake katika kilimo cha kisasa chenye tija na mchango mkubwa katika uchumi wa familia na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wao, washiriki wa kikao hicho waliotoka katika taasisi za kidini, wawakilishi wa makundi maalum pamoja na asasi za kiraia, wameupokea mradi huo kwa moyo wa shukrani na kuahidi kuwa mabalozi wema wa kuhamasisha vijana kuomba kujiunga na mafunzo hayo ya muda mfupi yenye tija kubwa katika kujiajiri na kuchangia ukuaji wa uchumi wa mtu binafsi na taifa.

Kwa mujibu wa taratibu za mradi, sifa za kujiunga na mpango huo ni kwa raia wa Tanzania kutoka mikoa husika, wenye umri kati ya miaka 18 hadi 35 na wenye elimu kuanzia darasa la saba na kuendelea. Fomu za maombi zinapatikana kupitia tovuti ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) pamoja na katika ofisi za VETA za mikoa husika.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABORA YAZINDUA RASMI MRADI WA YEFFA KUWAWEZESHA VIJANA KIUCHUMI.

    January 29, 2026
  • UCSAF YABADILISHA USO WA MAWASILIANO MKOA WA TABORA

    January 28, 2026
  • RC CHACHA APOKEA UJUMBE WA ALN, WAUNGA MKONO JITIHADA ZA KUKUZA MAADILI NA KUPINGA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA KWA VIJANA.

    January 28, 2026
  • DKT.MBOYA APOKEA WAGENI KUTOKA UNICEF, WALIOFIKA KUFUATILIA MIRADI YA ELIMU INAYOFADHILIWA NA SERIKALI YA CANADA MKOANI TABORA.

    January 27, 2026
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa