• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

UCSAF YABADILISHA USO WA MAWASILIANO MKOA WA TABORA

Posted on: January 28th, 2026

Mkoa wa Tabora umeendelea kupiga hatua kubwa katika sekta ya mawasiliano baada ya utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali (DTP) unaosimamiwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), ambapo minara 50 ya mawasiliano ya simu na intaneti imejengwa kwa lengo la kuondoa maeneo yasiyo na mawasiliano na kupanua upatikanaji wa huduma hizo vijijini na pembezoni.


Kabla ya mradi huu, vijiji vingi mkoani Tabora vilikosa kabisa mtandao wa simu na intaneti, hali iliyowalazimu wananchi kusafiri umbali mrefu kupata huduma za msingi za mawasiliano, kifedha na taarifa. Baada ya utekelezaji wa mradi, vijiji 99 sasa vimeunganishwa na mawasiliano, hatua iliyoboresha kwa kiasi kikubwa maisha ya wananchi na shughuli zao za kiuchumi na kijamii.


Kwa mujibu wa takwimu za utekelezaji, mradi umehusisha wilaya zote saba za mkoa wa Tabora, kata 45 na vijiji 99, ambapo minara yote 50 iliyopangwa imekamilika kwa asilimia 100 na kuanza kutoa huduma, na kufanya Tabora kuwa miongoni mwa mikoa iliyopata idadi kubwa ya minara ya mawasiliano nchini.


Huduma hizo sasa zimefika hata katika maeneo magumu kufikika yakiwemo ya porini, yaliyo mbali na barabara kuu na pembezoni kabisa kama Ipole, Usunga na Ugunga, hali iliyoleta mafanikio ya kimkakati katika kufungua maeneo hayo kijiografia na kiuchumi.


Minara hiyo inahudumiwa na makampuni mbalimbali ya simu yakiwemo Airtel, Vodacom,Halotel,TTCL pamoja na Yas, hatua iliyoongeza ushindani wa huduma, kuboresha ubora wa mtandao na kupunguza gharama za mawasiliano kwa wananchi wa mkoa wa Tabora.


Kwa ujumla, utekelezaji wa mradi huu umeleta athari chanya ikiwemo kuongezeka kwa mawasiliano ya simu na intaneti vijijini, kuimarika kwa elimu kwa njia ya TEHAMA, kuboreshwa kwa huduma za afya kwa mifumo ya kidijitali, kukua kwa biashara, kilimo na ujasiriamali wa kidijitali pamoja na kurahisisha upatikanaji wa huduma za serikali mtandao.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • UCSAF YABADILISHA USO WA MAWASILIANO MKOA WA TABORA

    January 28, 2026
  • RC CHACHA APOKEA UJUMBE WA ALN, WAUNGA MKONO JITIHADA ZA KUKUZA MAADILI NA KUPINGA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA KWA VIJANA.

    January 28, 2026
  • DKT.MBOYA APOKEA WAGENI KUTOKA UNICEF, WALIOFIKA KUFUATILIA MIRADI YA ELIMU INAYOFADHILIWA NA SERIKALI YA CANADA MKOANI TABORA.

    January 27, 2026
  • WAZIRI SHEMDOE ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO YA SH. BILIONI 17.2 MKOANI TABORA, ATOA WITO IKAMILIKE KWA UBORA NA KWA WAKATI

    January 25, 2026
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa