Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani amewaongoza mamia ya wananchi wa manispaa ya Tabora katika Uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti inayoitwa "Maji ni uhai na mti ni maisha " aliyoizinduwa tarehe 01.01.2023 katika kituo cha Afya Maili Tano.
Katika uzinduzi huo wa wenye kauli "Maji ni uhai na miti ni maisha" Dkt. Batilda alipata nafasi ya kupanda mti ikiwa ni ishara ya uzinduzi huo. Aidha ametembelea wodi ya wazazi ambapo alifanikiwa kuwatembelea Watoto waliozaliwa usiku wa kuamkia tarehe 01.01.2023 Ambapo napo aliwajulia hali Watoto hao na kisha kutoa zawadi ya sabuni, sukari na vitu vingine na kuwapa salamu za mwaka mpya kutoka kwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kwenye hotuba yake, Dkt. Batilda ameweza kufafanua oboreshwaji katika sekta ya afya mkoani Tabora ambapo hospitali 5 za wilaya na shule mpya 12 zilijengwa kwa mwaka 2022.
Lakini pia amewaomba TFS pamoja na wadau wa mazingira kutoa elimu ya mazingira kwa wananchi ili kuweza kuendeleza zoezi la upandaji miti mkoani Tabora.
Aidha, Mkuu wa Mkoa , kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Tabora alimshukuru Mh. Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kuweza kutoa fedha ambazo zimeendelea kuleta miradi mingi ya maendeleo mkoani Tabora.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa