• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WANANCHI WA MKOA WA TABORA TUCHUKUE TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA MPOX: KINGA NI BORA KULIKO TIBA - DKT. MBOYA.

Posted on: March 16th, 2025



Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, ameongoza kikao kilichohusisha wataalamu wa afya ngazi ya mkoa na waandishi wa habari kuhusu tahadhari dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa mpox (monkeypox) nchini. Dkt. Mboya amewataka viongozi wa halmashauri zote kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu hatari ya ugonjwa huu na jinsi ya kujikinga.

Akitoa elimu ya kina kuhusu ugonjwa wa mpox, mratibu wa tiba wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Benedict Komba, alieleza kuwa ugonjwa huu ni wa mlipuko na unasababishwa na virusi ambavyo awali vilianzia kwa wanyama na kuhamia kwa binadamu. Dkt. Komba alisisitiza kuwa ugonjwa huu unaweza kuambukiza kupitia hewa, kugusa majimaji ya mwili wa binadamu aliyeambukizwa, au kugusa maeneo yaliyoathirika.

Dkt. Mboya alisisitiza kuwa elimu kuhusu tahadhari lazima iendelee kutolewa kwa wananchi, lakini pia wananchi wanatakiwa kuchukua hatua za kujikinga dhidi ya ugonjwa huu, kama walivyofanya wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19. Aliwahimiza viongozi wa vijiji na vitongoji kutumia mifumo rasmi ya kiutawala ili kufikisha ujumbe wa tahadhari kwa wananchi.

"Ni muhimu wananchi watumie mifumo rasmi ya kiutawala ili kufikisha elimu ya tahadhari juu ya ugonjwa wa mpox. Ikiwa mgonjwa mwenye dalili za mpox atajitokeza, lazima apelekwe katika kituo cha afya ili apate matibabu sahihi. Waganga wa kienyeji wanatakiwa kuepuka kujihusisha na tiba za magonjwa ya mlipuko kwani zina hatari kwao na kwa wagonjwa," alisema Dkt. Mboya.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Honoratha Rutanisibwa, aliwatoa hofu wananchi, akisisitiza kuwa mkoa wa Tabora uko salama kwa sasa. Alieleza kuwa hakuna taarifa rasmi kutoka kwa wataalamu wa afya zinazothibitisha uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa mpox mkoani Tabora, lakini alitoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari.

Tahadhari hii inakuja wakati mkoa wa Tabora ukiwa ni moja ya mikoa inayopokea wageni wengi kutoka mikoa jirani ya Kigoma, Katavi, Singida, na Shinyanga, ambayo inapakana na nchi jirani za Congo, Rwanda, na Burundi. Hii inafanya muingiliano wa watu kuwa mkubwa, hasa kwa shughuli za kibiashara na usafirishaji. Hivyo, wataalamu wa afya wanasisitiza umuhimu wa kuchukua tahadhari ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa mpox.

Endelea kuchukua tahadhari ili kulinda afya yako na ya wengine.












Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa