• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WANAWAKE JITOKEZENI KWA WINGI KUGOMBEA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI,KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MWAKA 2025 – DKT. MKANACHI.

Posted on: March 8th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Dkt. Khamisi Mkanachi, amemuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Tabora,Mheshimiwa Paul Chacha katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake yaliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Mji, katika Uwanja wa Samora.

Akihutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo, Mheshimiwa Mkanachi ameipongeza ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tabora kwa usimamizi mzuri wa mikopo ya asilimia kumi, ambapo kati ya shilingi bilioni 3.9, wanawake wa mkoa wa Tabora wamewezeshwa shilingi bilioni 1.9 kupitia vikundi 226.

"Ndugu zangu, sisi katika Mkoa wa Tabora tumefanya jitihada mbalimbali kuhakikisha haki, usawa, na uwezeshaji wanawake unakwenda vizuri. Kuanzia Januari 2024 hadi Februari 2025, mikopo ya asilimia kumi yenye thamani ya shilingi bilioni 3.9 imetolewa, ambapo vikundi vinavyohusisha wanawake 226 vimepata fedha hizo. Wanawake pekee wamepokea bilioni 1.9, vijana bilioni 1.7, na walemavu milioni 264.3. Na katika suala la urejeshaji wa mikopo, kina mama ni wepesi, na wanarejesha kwa ufanisi mkubwa. Hii ni hatua nzuri katika kuwawezesha wanawake, nawapongeza sana," alieleza Dkt. Mkanachi.

Vilevile, Mheshimiwa Mkanachi alitoa rai kwa wanawake kuzingatia suala la malezi ya watoto, akisisitiza umuhimu wa kudumisha maadili mema na kuzungumza na watoto ili kutambua changamoto wanazokutana nazo. Aliongeza kuwa mmomonyoko wa maadili unazidi kuongezeka, na hivyo ni muhimu kuwa na muda wa kuwasikiliza watoto na kuhakikisha wanapata malezi bora.

Aidha, alisisitiza matumizi ya nishati safi ya kupikia na kusema kuwa matumizi ya nishati mbadala ni bora na rahisi kuliko matumizi ya kuni na mkaa, ambayo yanahatarisha mazingira. Alitoa wito kwa wananchi kuwa tayari kukubali mabadiliko haya, kwani dunia nzima inahama kwenye matumizi ya nishati zinazodhoofisha ustawi wa watu kwa kutumia nishati mbadala.

Mhe.Mkanachi pia alisisitiza umuhimu wa wananchi kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu, akiwataka wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ili kufanikisha usawa na uwakilishi wa wanawake katika vyombo vya maamuzi.

Akitoa salamu kwa niaba ya wabunge wa Mkoa wa Tabora, Mheshimiwa Margaret Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo, alisisitiza kuwa ili kufikia usawa ambao wanawake wanaupigania, ni muhimu kuzingatia suala la elimu. Alieleza kuwa bila maarifa, ni vigumu kufikia usawa wa kimaendeleo, hivyo ni jukumu la kila mwanamke kujiendeleza kielimu ili kusaidia mapambano ya ukombozi wa wanawake nchini.

Maadhimisho hayo yalihitimishwa na Mhe. Mkanachi kwa kutoa vyeti vya pongezi kwa makundi mbalimbali ya wanawake mahili na wadau waliofanikisha shughuli muhimu ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa