Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Pof. Adolfu Mkenda amewahakikishia watanzania kuwa, Serikali inatambua misingi ya elimu jumuhishi ili kuwapa nafasi wanafunzi wenye mahitaji maalumu kusudi wasiachwe nyuma. Ameyasema hayo alipokuwa akihutubia kwenye mahafali ya Tisa (9) ya Chuo Kikuu Cha Askofu Mkuu Mihayo Tabora (AMUCTA) kwenye viwanja vya AMUCTA vilivyopo Manispaa ya Tabora. Novemba 25, 2023.
“Ushirikishwaji katika elimu sio tu jambo la maadili na hiari, bali ni haki msingi ya binadamu. Lazima tuhakikishe kuwa kila mtu, bila kujali uwezo wake wa kimaumbile au kiakili, anapata elimu bora” alisema Waziri Mkeda
Waziri Mkenda ameeleza kuwa, licha ya kuwa na changamoto kwenye utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kati, bado Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imejidhatiti kwenye kuhakikisha wanafunzi wote wanaokwenda chuo wanapata mikopo bila kujali chuo cha Serikali au binafsi.
“Ni imani yangu ongezeko la wanachuo wanaonufaika na mikopo ya Elimu ya Juu na sasa stashahada, ni jitihada mahususi za Rais wetu za kuongeza wigo wa kupata elimu kwa watanzania” Alisistiza Mhe. Waziri
Aidha, Profesa Mkenda amefafanua kuwa, Serikali inatambua mchangoa wa Taasisi za kidini na sekta binafsi kwenye utoaji wa elimu bora kwa kuweka misingi imara ya utoaji wa elimu jumuhishi na mfano mzuri ni Chuo Kishirikishi cha AMUCTA kilichopo Mkoani Tabora.
“Kipekee napenda kuwahakikishia kwamba Serikali inatambua mchango wa Chuo Kikuu Kishiriki AMUCTA kwa kuwa kinara katika kuwekeza zaidi katika kuweka mazingira ya kujifunzia na kufundishia kuwa jumuishi” alisema Profesa Mkenda
Naye, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Peter Bura akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, ameeleza kuwa uongozi wa Mkoa unatambua mchango mkubwa unatolewa na Chuo Kishirikishi cha AMUCTA kwenye utaoji wa elimu jumuhishi kwa kuwaandaa walimu ambao wanakwenda kuwatumikia watanzania.
Mahafali ya Tisa (9) ya Chuo Kikuu Cha Askofu Mkuu Mihayo Tabora (AMUCTA) yaliofanyika katika viwanja vya AMUCTA vilivyopo Manispaa ya Tabora yalihusisha jumla ya wanafunzi wahitimu 357.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa