• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI TABORA KWA KUKAGUA NA KUWEKA MAWE YA MSINGI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 7

Posted on: March 13th, 2025

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amehitimisha ziara yake ya siku mbili mkoani Tabora kwa kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi minne muhimu yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 7. Miradi hii inatekelezwa katika Halmashauri ya Nzega Mji na Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kuharakisha maendeleo katika mkoa wa Tabora.

Akitoa salamu za mkoa, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Cornel Magembe, aliishukuru Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuleta fedha nyingi za miradi ya maendeleo katika mkoa huo. Alisema kuwa fedha hizo zimeboresha huduma za elimu, afya, na miundombinu, na hivyo kurahisisha shughuli za uzalishaji na kuboresha maisha ya wananchi wa Tabora.

Wabunge wa jimbo la Bukene, Mhe. Selemani Zedi, na jimbo la Nzega Vijijini, Mhe. Hamisi Kigwangala, walieleza shukrani zao kwa serikali kwa kuleta fedha za miradi ya maendeleo. Walitaja mafanikio makubwa yaliyopatikana kutokana na usimamizi mzuri wa miradi hiyo, ikiwemo kuboreshwa kwa huduma muhimu za kijamii na miundombinu katika wilaya ya Nzega na mkoa mzima wa Tabora.

Kwa upande wake, Mhe. Majaliwa aliwahakikishia wananchi wa Tabora kuwa serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ipo imara na itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kwa lengo la kuboresha maisha ya Watanzania. Alifurahishwa na kasi ya maendeleo iliyopatikana katika majimbo ya Nzega Mjini, Nzega Vijijini, na Bukene, akitaja kuwa ni matokeo ya usimamizi mzuri wa wabunge na ushirikiano kati ya Chama na Serikali katika mkoa wa Tabora.

Ziara ya Mhe. Majaliwa ilihitimishwa kwa kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi minne mikubwa ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na: Mradi wa ujenzi wa stendi ya mabasi katika Halmashauri ya Mji wa Nzega unaogharimu shilingi bilioni 4.2, Ujenzi wa shule ya amali ya Makomero yenye thamani ya shilingi bilioni 1.6, Ujenzi wa kituo cha afya Itobo chenye thamani ya shilingi milioni 500 pamoja na ujenzi wa shule mpya ya ufundi Mbagwa, ambapo mradi mzima unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 1.6.

Miradi hii ni uthibitisho wa dhamira ya serikali katika kuboresha sekta za elimu, afya, na miundombinu, na itaendelea kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya mkoa wa Tabora na nchi kwa ujumla.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa