• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WAZIRI WA AFYA AONGOZA MAADHIMISHO YA WIKI YA CHANJO KITAIFA TABORA,

Posted on: April 28th, 2025

Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, ameongoza maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Tabora katika maadhimisho ya Wiki ya Chanjo Kitaifa yaliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Uyui. Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wakiwemo wananchi na wadau wa afya kutoka maeneo tofauti ya mkoa huo.

                                  

Katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Deusdedith Katwale, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Mhe. Paul Chacha, alitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya uliosaidia kuboresha miundombinu na kuongeza upatikanaji wa dawa katika hospitali za mkoa huo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Dkt. John Mboya, naye alitoa shukrani kwa serikali kwa uwekezaji wa zaidi ya shilingi bilioni 30.2 katika sekta ya afya. Alifafanua kuwa hadi kufikia Machi 2025, upatikanaji wa dawa mkoani Tabora umefikia asilimia 84. Aidha, aliwasisitiza watumishi wa afya kuendelea kuwajibika kwa kuzingatia maadili ya taaluma zao na kuwa mfano wa utoaji huduma bora kwa jamii.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania, Dkt. Charles Sagoe-Moses, aliwahimiza wazazi na walezi kushiriki kikamilifu katika kampeni za chanjo ili kusaidia kuokoa maisha ya wananchi. Alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa jamii katika kuhakikisha chanjo zinawafikia walengwa wote kama njia ya kuimarisha afya ya umma.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, alibainisha kuwa mwaka huu wa maadhimisho ni wa kipekee kwani unatimiza miaka 50 tangu Tanzania ianze rasmi matumizi ya chanjo mbalimbali. Alieleza kuwa taifa linaendelea kuimarisha huduma za chanjo ili kupunguza vifo, kuzuia ulemavu na kulinda afya ya wananchi kwa ujumla.

Aidha, Waziri Mhagama alitaja magonjwa kama ndui, kifaduro na dondakoo kuwa miongoni mwa magonjwa yaliyotokomezwa kupitia kampeni za chanjo. Alitoa wito kwa wananchi kufuata ushauri wa wataalam wa afya, kubadili mitindo ya maisha, na kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya mlipuko na magonjwa yasiyoambukiza. Maadhimisho haya yamebeba kaulimbiu isemayo: "Kinga ni Tiba: Tuungane Kuwezesha Walengwa Wote Wapate Chanjo."

 

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WIZARA YA AFYA NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA TABORA YAENDESHA KIKAO ELEKEZI CHA MREJESHO WA MAFUNZO NA MAPITIO YA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

    May 14, 2025
  • JESHI LA POLISI TABORA LAPATA MAGARI 6 MAPYA KWA AJILI YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

    May 12, 2025
  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa